MATATIZO YA HEDHI NA SULUHU YAKE

MATATIZO YA HEDHI:

Matatizo ya Hedhi yanawagusa moja kwa moja

hata hivyo nayo yana tiba yake inayolingana na aina ya tatizo husika.

TIBA YA HEDHI ILIYOFUNGA (AMENERRHOEA):

Kanuni ya kwanza: Tafuna ufuta kiasi cha kijiko kimoja kila siku mara tatu. Fanya hivyo hadi upate hedhi. Ni bora zaidi kula ufuta kabla ya zile siku ambazo hedhi hutoka na uendelee wakati inapotoka hedhi. Dawa hii ni hatari kwa mwanamke mja mzito, hivyo atahadhari nayo,na tangu hapoyeye haimuhusu.

TIBA YA HEDHI ISIYOTOKA VIZURI: Chukua Jirjir (rocket) kijiko kimoja ukoroge ndani ya kikombe cha maji ya moto. Yakishapoa uchuje. Kunywa kikombe kimoja cha kahawa kutwa mara tatu.

TIBA YA HEDHI INAYOTOKA KWA WINGI ZAIDI YA ADA:

TIBA Kanuni ya kwanza Chukua kijiko kimoja cha maua ya Babunaji (Chamomile) ukoroge ndani ya kikombe kimoja cha maji ya moto. Yakishapoa, unywe kikombe kimoja kutwa mara tatu kabla ya kula.

TIBA YA MAUMIVU YA HEDHI YANAYOTOKA KIDOGOKIDOGO (DYSMENORRHOEA):

Tiba: Chukua Nanaa na utayarishe mfano wa chai. Kunywa kikombe kimoja cha chai kutwa mara tatu.

Tiba ya Pili: Chukua mvuje wa kidonge (kidonge kimoja ) na unga wa pilipili manga (black Peper) gramu 50. Weka dawa hizi mbili ndani ya glasi moja ya maji kisha uifunike na uiache ilowane. Bila ya kuchuja kunywa kijiko kimoja kikubwa kutwa mara moja .Rudia tena kunywa siku ya pili ikiwa hujapata mabadiliko.Dawa hii huzibua hedhi iliyoganda au kufunga.

TIBA YA HEDHI INAYOCHELEWA KUTOKA KWA SIKU ZAKE AU KUTOKA KABLA YA SIKU ZAKE KUFIKA

Hapa maana yake ni kuwa baina ya hedhi mbili huenda yakakaribiana sana au kuachana sana kinyume na ada. Yaani siku za tarehe zake haziendi sawa Chukua bakdonise (parsley) gramu 50 kisha uweke ndani ya maji lita moja, ichemshe kwa muda wa dakika tano na ikishapoa uchuje. Kunywa glasi moja kutwa mara mbili.

Comments

Popular posts from this blog

MAFUSHO MADINI YA KILA NYOTA NA JINSI YANAVYOTUMIKA

NDOTO ZA FEDHA NA TAFSIRI ZAKE UKIOTA UMEOKOTA HELA. UKIOTA UMEDONDOSHA HELA. UKIOTA UNAPEWA HELA

FAHAMU KUHUSU MTI NDULELE TURA FAIDA NA MATUMIZI KATIKA AFYA NA MAPENZI