TIBA MAALUMU YA MAFUA NA MAPAFU KWA AJILI YA WATOTO



NAAM leo nitazuzngumzia kuhusiana na watoto. Juma lililopita nilizungumzia kuhusiana na mtoto anayelia usiku. Mashallah wengi waliofanya wamenitumia ujumbe kuwa watoto sasa wanalala vizuri.


Mara nyingi kila kabila lina utaratubu wake juu ya dawa asili za kuwapa watoto ili wapite kwenye zile hatua za ukuaji pasina matatizo yoyote hapa nazungumzia kukaa, kutambaa, kusimama, kutembea, kukimbia na kuota meno wakati mwingine kuchangamka.

Kwetu Tanga mtoto anapokuwa mchanga huoshwa na mavuo maalumu na kupewa dawa za kunywa za miti shamba ni miti ya aina saba na magome ya mti fulani na pia hupewa dawa za kunywa za miti minne maalum akitoka hapo km mtoto wakiume anakua mwanaume kweli kama wakikeanakuwa wakike kweli mliokutana na watu wa tanga mnanielewa zile shughuli zinaanza kupikwa utotoni.

Leo ntazungumzia kifua kwa watoto wadogo. Kifua kinaweza kusababishwa aisha mtoto kula uchafu wakati anazaliwa hii ni pumu. Lakini pia yaweza ikawa hali ya hewa na mambo mengine 

Dawa zake nimezigawanya katika sehemu mbili. Sehemu ya kwanza watoto kuanzia mwaka siku moja hadi mwaka mmoja, sehemu pili kuanzia mwaka hadi miaka 5

Kwa watotot wa changa
Kwanga watakiwa umuangalie ana tatizo gani yaweza ikawa maziwa unayompa hayapendi, au vyakula anavyokula mzazi vinamuathiri pamoja na vingine ikiwa ni pumu subiri atimize mwaka mmoja


Kama ni mafua na kifu cha kawaida  chukua punje kadhaa za vitunguu saumu zitwange ziwe laini kabisa kisha fuata taratibu zifuatazo kwa ufasaha
Mpake kweny unyayo wake mtoto kwenye kifua ila kifuani usimpake sana chukua mpake kiganja ambacho anapenda kukinyonya kidogo alafu jipake mzazi kwenye mikono umnusishe kwa mbali puani wakati unamnyonyesha paka juu ya maziwa yako sio kwenye chuchu anaponyonya

Wakati unamnyonyesha hakikisha ile alama nyeusi ya duara ya chuchu imeingia mdomoni mwake yote

Watoto juu ya mwaka
Tiba  Yake, chukua majani  ya  mpera kiasi  cha kama  viganja  vinne, yaponde  pamoja  na magome  ya  muembe 'ukipata mwembe tanga au dodo ni vizuri zaidi' kiasi  cha viganja  vinne, 
na  tunda  la  koma manga, twanga  vyote  kwa  pamoja  ( Yani majani  ya  mpera, magome  ya  muembe na tunda  moja  la  komamanga ).
Ukisha  maliza  kutwanga, changanya  na  maji  lita mbili  halafu  chemsha  pamoja na lita  moja  ya  asali mbichi  ya  nyuki  wadogo. 
 
Chemsha  hadi  itokote, halafu  ipua  dawa  yako
 
 Matumizi : Kwa  mtoto  mdogo mwenye  umri wa  kati ya  mwaka  mmoja na  miaka  mitano, tumia  kumpa  kijiko kimoja  kikubwa  mara  mbili kwa  siku, asubuhi  na  jioni n  kwa  siku  saba.

Hii hata kwa watu wazima wanaosumbuliwa na kifua hutumia vijiko viwili vya chakula mara mbili kwa siku ndani ya siku 21.
Wabillah tawfiq
www.tabibuasili.blogspot.com

Comments

Popular posts from this blog

MAFUSHO MADINI YA KILA NYOTA NA JINSI YANAVYOTUMIKA

NDOTO ZA FEDHA NA TAFSIRI ZAKE UKIOTA UMEOKOTA HELA. UKIOTA UMEDONDOSHA HELA. UKIOTA UNAPEWA HELA

FAHAMU KUHUSU MTI NDULELE TURA FAIDA NA MATUMIZI KATIKA AFYA NA MAPENZI