Posts

Showing posts from 2020

KUHUSU KUNG'ARISHA NYOTA KWA KUTOA SADAKA KWA WATOTO WADOGO

Image
KUJIIMARISHA KINYOTA MVUTO WA CHUMO LA AMALI ZAKO KILA mmoja anazo shughuli zake za kujitafutia ridhki ili kuyaendesha maisha yake. Zipo shughuli za heri na shari ila si wote wanaofanya shari hupenda wakati mwingine ni majukuku kuwabana na hakuna njia nyengine ya kuyatatua. Si hamasihi watu kufanya shughuli mbaya nipo katika kukuelewesha namna ya kuupata unafuu katika mihangaiko yako. Nmekuwa nikiulzwa sana baadh ya maneneo ninayotumia kuna watu huwachanganya ila hiki ninachoandika ni kiswahili sanifu alhamdulillah nmekaa na wazee pia nmesoma sana kiswahl elimu ya dunia. Hapo juu neno chumo maana yake ni kipato au fedha unayoipata baada ya kufanya kazi amali ni shughuli yoyote unyoifanya ili kupata hicho kipato sasa kuna amali njema na mbaya kama nilivyoeleza hapo. Kabla ya kuendelea nataka niweke sawa ikiwa una mikwamo mambo hayaend unahs na kuona kabisa sio kawaida kwanza yatakiwa iangaliwe tatzo na chanzo chake ikiwa ni vifungo husda upepo mchafu majini nk vishughulikiwe

MAFUSHO MADINI YA KILA NYOTA NA JINSI YANAVYOTUMIKA

Image
KATIKA uchambuzi wa Nyota ninazozitoa asubuhi huwa nazungumzia mafusho ya Nyota. Naweza nikaweka maelezo alaf kwenye ushaur nikasema leo watakiwa ufushe fusho la nyota yako kabla ya kuanza shughuli yako. Makala haya yataaangazia juu ya fusho la kila nyota na utumizi wake. Anayekuletea uchambuzi hii ni Mtabibu ASILI TZ. Niliwashatoa makala za uchambuzi wa kila nyota. Zile nyota kumi na mbili kuanzia Punda mpaka Samaki, nilifafanua siku zao za bahat, watu wa kushirikiana nao siku mbaya kwao, malaika na majini wa nyota zao pete vito na shughuli au kazi za kilufanya ili uendane na nyota yako na kujipatia kipato. Makala hizo zipo peruz post za nyuma utaona ukiutaka uchambuz binafs utanilipa ili nikufafanulie kama utaona kazi kusoma post za nyuma. Fusho ni dawa ambayo hutumika kuchoma aidha kwa kujifusha yaan kujifunika ili moshi ukiungie mwilini au kuchoma kawaida. Hutunika katika shughuli mbalimbalu hasa za kuvuta ridhki kutoa uzito kuleta wepes pamoja na masuala ya kimapenzi.

FAHAMU KUHUSIANA NA PETE ZA BAHATI ZINAVYOLETA MVUTO

Image
VITU AMBAVYO HUTAKIWI KUVICHUKULIA POA ILI KUFANIKISHA MALENGO YAKO KILA asubuhi huwa naweka post inayohsiana na utabiri wa Nyota yako wa kutwa nzima. Kuna vipengele vingine vianaonesha hali itakavyokuwa wiki nzima. Katika ufafanuzi huo kunakuwa na ushauri ndani yake wa kinyota. Ikiwa kile kinachoandikwa kinafanana kabisa au ni chakweli kwako katika Nyota yako jitahd kufuata ule ushaur. Nmegundua wengi mnasoma nakuacha kisha likikukuta ndo unaanza kutafuta pakutokea napokea sana jumbe za namna hiyo ninachowashauri jitahdini kufuatilia kwa kina maelezo ya nyota zenu. Uchambuzi huu unaletwa kwako na Mtabibu ASILI TZ. Hutakiwi kuchukulia poa Ndoto zako, ikiwa unafulululiza ndoto zenye ishara fulan jitahf kufuata ushaur unaopewa kitaalam. Siku za usoni inaweza kuwa hatari zaid. Mfano umeelezwa kuwa ni ishara ya vifungo mkwamo wa jambo na si mara moja, ishara ya uchawi wa kulishwa au kutolewa, ishara ya jini mahaba, ishara ya mizimu au majini wabaya na ndoto nyengine ambazo kwa

KUHUSU VUMBI LA KONGO KASONGO MUNDENDE UHALISIA NA MATOKEO YAKE

Image
NIMEONA nilizungumzie hili swala baada ya kupata jumbe nyingi zikiulizia kuhusiana na hasa na dawa zinazopewa jina la vumbi la kongo chakupaka kasongo mundende na majinaengine. Wapo waliowahi kuzungumzia madhara ya madawa haya hasa baada ya matumizi ya muda mref. Mimi nitagusia kitaalam zaid si biashara, nakumbuka niliwah kuzungumzia kuhusiana na SHABU faida n madhara yake pamoja na vipipi hasa kwa wanawake peruz post zilizopita kama umepitwa na darasa hzo. Chambuzi hizi zinaletwa kwako na Mtabibu ASILI TZ. Utandawaz umeleta urahisi wa mambo mtu unaweza kutafuta kitu kwa mtandao na ukakipata. Ukiitumia vizur inaweza kukuleta faida kama unavyosoma darasa zangu ingelikuwa hakuna njia za mawasiliano na mitandao ingekupasa uje ofisin ili kupata ufafanuzi pia nisingeweza kumudu kufafanua kwa watu wote nyinyi endpo mngekuja mmoja mmoja. Watu wengi wamekumbwa na upepo wa vitu vinavyovuma. Vipo vitu vyenye faida na vipo vyenye madhara sio vyote ni vibaya. Tufahamu uhalisia wake fai

NYOTA ZENYE TABIA 'ASILI' YA UDONGO UHALISIA MAFANIKIO NA USHIRIKIANO WAKE

Image
HII ni makala ya nne na ni ya mwisho katika ile orodha ya Tabia au asili ya Nyota. Tulianza na Nyota zenyewe zipo kumi na mbili nikazichambua moja baada ya nyengine maana yake tabia zake matendo siku za bahat namba za bahat nani ushirikiane nae nyota gani ni mbaya kwako, bishara gani ufanye mapambano gani utumie. Kila rangi ina nguvu yake kinyota kuna rangi ni za mapenzi kuna rangi ni kwa ajili ya fedha kuna rangi kwa ajili ya nyumba au eneo lako la biahsara yote niliyazungumza katika kila Nyota niliyoitaja anayekuletea chambuzi hizi ni Mtabibu ASILI TZ. Wale mnaotaka uchambuzi kwenye coment mtanishamehe siwez kukuwekea ufafanuz uliopita  wote kwenye coment makala zipo zitafute hapa soma ninachoweza kukusaidia hujui nyota yako naweza kukusaidia kukitajia lakini uchambuzi soma post zilizopita maana ni maneno maref ila ukiona kazi kusomasoma post zilizopita tutafanyiana private utanilpa nitakupatia uchambuzi inbox. Tulishazungumza tabia za MOTO, UPEPO na MAJI leo tutamaliza n

JINSI 'NJIA' YA KUJUA KUNDI LAKO LA NYOTA KUOITIA HERUFI YA JINA LAKO KWA WSIOJUA TAREHE ZAO ZA KUZALIWA

Image
MFUMO WA KUJUA NYOTA YAKO KUPITIA YA KUZALIWA KUPITIA HERUF YA KWANZA YA JINA LAKO Hii kwa wale wasiojua tarehe zao za kuzaliwa, kwa sababu mfumo wa Nyota huletwa na tarehe yako ya uzawa yaani siku ulioyzaliwa, saa na siku. Katika mfumo wa Nyota kila siku kuna SAYARI, MALAIKA na MAJINI wanaotawala hizo siku. Siku utakayizaliwa itabebwa na hvyo vtu ndivyo vutakuwa vinakupa muongozo wa nini ufanye nini usifanye maisha yako yatakuawaje na hata watu wakushirikiana nao kibishara na kindoa. Sasa wale wasiojua tarhe angalia njia hapo chini ili kujua herufi ya jina lako ipo lwemye kundi gani na vipi tunayapata na kuyachambua hayo majina. Hata wewe unayefahamu tarhe kunaambo nitakuja kuyazungumza mbele kwahyo nakili hili darasa weka kwenye kumbukumbu zako kwa sababu nikija kutoa maelezo siku nyengine nitaanzia nilipoishia na si kutoa njia hizi tena. Tafuta kalamu na karatasi au 'note book' kitunza kumbukumbu uhakikishe unanakiri hizi heruf sababu itakufaa mwenyewe somo litakapopita. TUF

NYOTA ZENYE TABIA 'ASILI' YA MAJI UHALISIA MAFANIKIO NA USHIRIKIANO WAKE

Image
TUPO kwenye muendelezo wa darasa zinazohusu masuala ya Nyota na taratibu zake. Masomo ya awali nilishazungumzia kuhusiana na kuitambua Nyota yako kwa tarahe uliyozaliwa pia nikatoa ufafanuz kuhusiana na Majina kwa wale wasiojua tarhe zao. Nakumbuka nishaongelea ufafanuz wa kila nyota tabia zao siku zao za bahat watu wakushirikiana nao siku za kufunga ndoa. Tabia z mbili za Nyota tayar nishazizungumzia MOTO na UPEPO na leo nitaongelea tabia ya MAJI kama ulipitwa na makala zilizpota kwenye ukurasa wangu Mtabibu ASILI TZ Nyota zipo kumi na mbili katika mdumo wake na zimebebwa katika tabia au asili nne bazo ni MOTO, MAJI UDONGO NA UPEPO. Makundi haya ndiyo yanayoleta muongozo nani ushirikiane nae na nani usishirikiane nae. Kuna ushirikiano wa kibiahsra kuna mahusiano ya kimapenzi. Hivi ni vitu viwili tofaut unavyopaswa kuvifahamu kiundan. Mashirikiano ya kikawaida hayafungamani na mashirkiano ya kimahaba mapenzi hivyo ukitaka kuangalia kuhusiana na muunganiko wa mapenzi watakiw

NYOTA ZENYE TABIA YA UPEPO UHALISIA, MAFANIKIO NA USHIRIKIANO WAKE

Image
TUNAENDELEA na uchambuzi wa tabia za za Nyota leo tupo kundi la UPEPO. Nishafafanua kuhusiana na MOTO, nishaeleza makundi yote ya Nyota kwa tarehe na Majina kwa wale wasiojua tarhe zao. Kama umepitwa soma post zilizopita. Ikumbukwe kwamba makundi ya Tabia za Nyota yapo manne nayo ni MOTO, UPEPO, MAJI NA UDONGO. Makundi haya ndiyo yanayoleta taswira nani ushirikiane nae nani uoe. Kuna vtu ukivikosea inakuwa kama ujenzi wa nyumba unapokosea msingi basi nyumba nzima haitakaa sawa. Msingo wa maisha wa mwanaadamu inabebwa na Nyota yake ya kuzaliwa. Na nyota ni ile siku ulipozaliwa siku saa na tarhe. Mfano siku ya leo ni Jumanne Sayar yake ni Mirikh watoto watakaozaliwa leo mfumo wa maisha yao yataendana na Sayar hyo kupitia tarhe yake ambayo itanuongoza kinyota. Kundi la UPEPO linabebwa na Nyota za Mapacha, Mizani na Ndoo. Watu wa Kundi hili wanaendana na kundi la MOTO mashirikiano kibiashara ilibupate faida. Kuna wakati unaweza shirikiana na kundi la UPEPO lenyewe ila kuna baad

NYOTA ZENYE TABIA YA MOTO UHALISIA, MAFANIKIO NA USHIRIKIANO WAKE

Image
TUPO kwenye muendelezo wa darasa zinazohusu masuala ya Nyota na taratibu zake. Masomo ya awali nilishazungumzia kuhusiana na kuitambua Nyota yako kwa tarahe uliyozaliwa pia nikatoa ufafanuz kuhusiana na Majina kwa wale wasiojua tarhe zao. Nakumbuka nishaongelea ufafanuz wa kila nyota tabia zao siku zao za bahat watu wakushirikiana nao siku za kufunga ndoa.  Makala ya jana nilizungumzia tabiabza Nyota ambazo zipo katika makundi manne niliyataja sasa tunaanza kuyacuambua kundi moja moja ikiwa umepitwa na maelezo niliyoyatoa hapo juu tafadha soma post zilizipita nishazifafanua ukihitaji uchambuzi private utachangaia gharama. Njia rahs na bura soma post zilizopita kumbuka chambuzi hizi zinaletwa kwako kupitia page ya Mtabibu ASILI TZ. Makundi niliyoyazungumza jana ni MOTO, MAJI UDONGO NA UPEPO. na nikaorodhesha kila kundi na nyota zake. Leo tutaanza na kundi la moto kadri siku zinavyozid kwenda tutazidi kuzichambua mpaka tuyamalize usisahau kila asubuh pitia gage yangu mtabibu

NATUMIA MADAWA LAKINI SIPATI MATOKEO FAHAMU UNAPOKOSEA NJIA ZA KUMALIZA MATATIZO SUGU

Image
LEO nmeona nitolee ufafanuzi hili suala baada ya kupokea maswali mengi kuhusiana na maelezo ya dawa hasa yanayotolewa mitandaon. Maswali mengi yanauliza kuhusu madawa yanaoelezwa kisha watu kuyatafuta kwenda kutumia lakini kile kilichoelezwa na matarajio huwa ni tofauti. Makala haya uyasome kwa umakini ujue unapokosea ni wapi ili urekebishe na hii hata kwa matabibu pia inawafaa, ufafanuzi huu unaletws kwako na Mtabibu ASILI TZ. Nitaweka makundi kadhaa kwa uchache ili upate kufumbua macho. Kwenye tiba asili ama Uganga kuna vtu viwili kwanza kuna maradhi ya kawaida na maradhi ya kichawi. Maradhi ya kawaida ni kama kuumwa kichwa ngiri chango degedege, malaria, tyfoid pumu nk. Nmetaja maradhi machache ili kuepua muda. Maradhi kama haya huwa yanatibika kirahisi hata nikikuambia kachume mti wa mvuje chemsha kwa ufupi kama zile makala ninazozitoa za miti na maradhi kwa watoto. Hizi haziihtaji utaalam unaweza ukasoma kitu ukaenda kitafuta ukafanya na ukapona muhimu kufuata maelezo

FAHAMU KUHUSU TIBA YA MARADHI YA DEGEDEGE KWA WATOTO

Image
MARADHI ya degege huwasumbua sana watoto kuanzia umri wa miaka 15 mpaka mwez mmoja. Marafhi haya hutofautiana kulingana na umri wa mtoto. Watu wazma wenye watoto zaid ya mmoja au waliowahi kuishi eneo lenye watoto wengi watakuwa wanaufahamu huu ugonjwa. Leo nitaongelea dawa ya kutuliza na kutibua tatzo ili lisijirejee tena. Kuna watoto wakikumbwa na tatzo hili kwa haraka mfushe kwanza na kumuogesha mti wa muinga jini mkunde pori mti ndio huo huo mmoja. Kwa tiba fuata maelezo hayo chini. Chukua  mvuje, mavi  ya Tembo, Majani ya vitunguu saumu yaliyomenywa na watu wengi ukipata ya shughulini ni vizuri zaidi. Mfushe kwa siku tatu mfululizo mara mbili kwa siku mtoto atakaa sawa Mtoto anayelia usiku au anastuka akiwa usingizin unamfukiza kabla ya kulala.  na pia ukiwa unamaumivu ya kichwa au kipandauso kinakusumbua unajifukiza au unanusa ule moshi. Pia fusho hilo huweza kukata damu puani. Mtu aliyekumbwa na upepo ubaya umeenda safar ghafla umefuka hujielewi. Au unaona hali tofau

UKWELI KUHUSU KISOMO CHA ALBADIRI 'AHLUL BADRI' MASHART USOMAJI NA MATOKEO YAKE

Image
NIMEPOKEA masuali mengi kuhusiana na hivi visomo vya albadiri. Leo nitautoa ufafanuzi juu ya hivi visomo vya albadiri. Visomo hivi vimegawanywa katika mafungu mengi kulingana na elimu ya mfanyaji na dhumuni la mfanyiwa, vimepewa majina ya kitaalam hapa nitaongea kwa ufupi maana ni mada pana inyohitaji muda elimu na utayar ufafanuzi huu unaletwa kwenu na Mtabibu ASILI TZ. Kama ulishawah kusikia kuhusiaba na albadiri bayana hii hufanywa kwa kubainusha jambo. Mfano umefanyiwa dhulma kuchukuliwa mke mume au kuibiwa ila hutak kudhuru unataka kumbaini mbaya wako ndio husomwa. Kuna albadiri za kuua kutia watu vichaa, kusafirisha watu kwa wapumbaza akili na kuna za kukinga aidha mwili nyumba eneo la biahsra shamba mali nk. Huo ni ufupi tu na kila jambo hapo juu lina mafanyo yake na nia zake katika ufanyaji wake. Mahitaji ya visomo hivi hushabihiana hukosana seh ndogo aidha idadi ya vifaa au rangi za wanyama wanaotumika katika kipengele cha kafara. Tufahamu walau kwa uchache mahitaj

MIZIZI YA MKUNAZI KATIKA TIBA ASILIA ZA UCHAWI NA KINGA YA NYUMBA NA MWILI

Image
MIONGONI mwa miti inayoheshimiwa na wwchawi basi mkunazi pia umo. Panapopandwa mkunazi mwanga hupitia mbali eneo hilo. Moja kati ya maajabu yake mtu mwenye roho mbaya ama husda hawez panda mti huu na ukamuotea. Leo tuangalie mzizi wake huko nyuma nishaongelea magome na majani pekua post zilizopita ikiwa ulipitwa, anayekuletea darasa hizi ni Mtabibu ASILI TZ. Mizizi ya mti huu ni mizuri hasa kwa maradahi yanayotokana na sihiri yaan uchawi uwe wakulishwa au wakukanyaga au wakukumba mti huu unaweza kukusaidia. Kwa mtu ambaye amekumba vtu vibaya mwili hauelew au mtu kaja ghafla haongei povu linamtoka achemshiwe mzizi wa mti huu pamoja na miziz ya mzaituni kisha achemshiwe majani ya mkunazi yachanganywe na mvumbasi na majani ya muingajini au wengine huuita mkundekunde au mkunde por ni mti mmoja kasoro majina. Mchemsho wa majani kamagonjwa anaweza kutembea mwenyewe akaoge au mumwagie kama kapoteza faham kisha mumpe mchemsho wa mizizi anywe atapata fahamu baada ya hapo muendelee n

UFAFANUZI WA NYOTA YAKO YA UZAWA, NYOTA ZINAZOENDANA KIMUUNGANO BIASHARA NA MAPENZI

Image
. MARA kadhaa nmekuwa nikieleza kuwa kuna makundi 12 ya nyota kulingana na miezi inayounda mwaka. Nyota hizi hutokana na tarehe ya uzawa ya muhusika. Wakat unazaliwa pale ndipo inapotengenezwa siri ya mafanikio yako kimaisha. Siku uliyozaliwa kuna Sayari inayomiliki hiyo siku tarahe yako kuna nyota inayomilik pia na saa. Kwa watu wenye elimu ya haya mambo hata jina wanakupa kupitia heruf zinazolete faida kwa kuoana vtu nilivyotaja hapo juu. Siku hizi watu wanawapa watoto wao majina ya wasanii kwenye sizon. Katika wiki kuna siku saba kila siku kuna sayar inayochomoza jua ndio tunazozitumia kutoa tabiri ya kila siku. ili upate unachotaka kwa wanaocheza michezo ya kubahatisha au kitu chochote lazma ujue nyota yako cku yako ya bahat saa yako ya bahat ndan ya ck hiyo na namba zako za bahati ukitumia kama ilivyo utapata utakacho.  Leo siongelei namba za bahati wala rangi nilishaongelea sana na kutoa formula yake. Bandiko litakufanya ujue nyota yako kikamilifu tafadhali kuwa makin

FAIDA NA MATUMIZI YA MAJI YA MVUA NA MPERA

Image
Hivi vtu viwili vna faida kubwa katika maisha ya mwanadamu. Vina faida kiafya, kazi, biashara, mvuto. Miaka ya nyuma kidogo niliwahi kuongelea mti wa Mpera niagusia faida zake nyingi kuanzia majani bakora yake matumda  na mizizi katika ulimwengu wa tiba za asili ikiwa ilikupita jitahdi kurejea post za nyuma kuna vitu vingi nmezungumza ambavyo vina faida kwako. Leo tutaangalia mvuto wa nyumba chumba na sehemu ya biashara kwa kutumia majani ya mpera na maji ya mvua. Maji ninayoyazungumzia hapa ni yale yanaytoka direct yaan weka chombo sehem ya waz sio maji yanayopitia kwenye bati au kitu chochote. Tafuta maji ya mvua yakuja direct ujazo wa lita moja. majani ya mpera machanga 21 hakikisha yawe ya mpera ule wa asili sio ile mipera ya kizungu ya madawa  Matayarisho yake Chukua hayo maji yagawe nusu Lita mara mbl. Twanga majani yawe laini kisha utaweka hayo nusu ya kwanza kwenye majani yachanganyane kisha uchuje maji na majani. Kisha utaongeza ile nusu lota ya pili kwenye hayo ma