MAGOME YA MTI WA MWAROBAINI TIBA KWA MAGONJWA NA JINSI UNAVYOTUMIKA



JUZI na jana niliongelea faiada za majani ya Mwarobain na asali yake. Leo nitaongelea kuhusiana na magome na mti wenyewe katika matibabu asili kwa mwili wa binaadamu. Mti huu unatibu maradhi mengi sana kama nilivyoeleza kwenye makala mbili za awali nilizozitoa. Ikiwa ulipotwa tembelea ukurasa wangu Mtabibu ASILI TZ.


Zamani wazee walikuwa wakiutumia huu mti kama mswaki na bado mpaka sasa kuna baadhi ua maeneo watu bado wanautumia kama mswaki. Moja ya faida zake unaweza kutoa hatufu mbaya mdomoni na kuua vijidudu vya ugonjwa wa meno. Ukiona dawa za meno kutoka nje zina neno limeandikwa herbal basi inatumika miarubain na mishibiri kutengeneza hizo dawa na huwa na rangi ya kijani.

Ukichukua magome ya mti huu ukayaanika ukatwanga upate unga wake, kwa wale wenye meno yenye rangi unatumia na mswaki kupigia utaweka na mafuta ya habbatsouda kisha unapigia inasafisha meno na kuyafanya kuwa meupe. Piga mara nyingi ili upate matokeo sio jambo la siku moja.

Kwa watu wanaoungua unaweza ukaweka unga kwenye maji ikawa kama tope kisha ukampaka mtu aliyeungua na moto. Pia anaweza kuweka kwenye maji yake ya kuoga na akatumia kuogea.

Ikiwa una matatizo ya ngozi ya muda mref koga maji uliyochanganya na unga wa magome ya mti huu. Shart yawe maji vuguvugu utaweka vijiko kadhaa ya unga wa magome ambao umesga au chemshia hayo maji na magome mazima kisha ipua toa yale magome poza maji nenda kaoge. Hii pia imashusha haraka mno.

Maswali weka hapo chini

Shida binafs niachie inbox

+255621442936

Comments

Popular posts from this blog

MAFUSHO MADINI YA KILA NYOTA NA JINSI YANAVYOTUMIKA

NDOTO ZA FEDHA NA TAFSIRI ZAKE UKIOTA UMEOKOTA HELA. UKIOTA UMEDONDOSHA HELA. UKIOTA UNAPEWA HELA

FAHAMU KUHUSU MTI NDULELE TURA FAIDA NA MATUMIZI KATIKA AFYA NA MAPENZI