Posts

Showing posts from September, 2020

TALASIMU YAKUKIDHI HAJA KUPATA KITU UNACHOKITAKA KWA WAKATI

Image
HUU NI WAQFU WA KILA KITU UNACHOKITAKA NA UKAKIPATA KWA WAKATI TARASIMU hii ni ya kukupa kile unachokitaka kwa wakati. Mfano unataka ndoa, au unataka kukopa pahala, au unataka ulipwe madeni yako chochote kile kasoro shughuli za mapenzi yaana kuvuta na kirejsha. Hii utaiandika siku ya ijumaa kama ni mwanaume angalia saa ya shamsi, kama ni mwanamke iandikwe wakati wa zuhra kwa zafarani nyekundu. Kisha upate kitambaa cha kijan cha hariri ikishaandikwa ipuliziwe udi au mafusho yanayoendana na nyota yako. Chini ya tarasimu hii itaandikwa dhumuni kama unataka ndoa itaandikwa dua au waqf wa ndoa kwa jina muhuiska mtakaji, ikiwa ni ridhi pia itaandikwa dua za kufungua ridhk kwa jina la mtakaji ikiwa ni kukopa kulipwa pia itaandikwa dua ya kutaka kitu kupata kwa wepes zipo kwenye vitabu vya muongozo. Ukishamliza utaiweka kwenye walet yako na utatembea nayo ikiwa mfuko wa kulia. Au niuzuri kama utaivaa mkono wako wa kulia hii ndani ya wiki utapata majibu kwa kile ulichokikusudia. Mwm

NDOTO ZA NDOA KUOA, KUOLEWA NDOTONI TAFSIRI NA MAANA ZAKE.

Image
NDOTO za harusi bimaana kuoa ama kuolewa zimetawaliwa na jini mahaba kwa silimia kubwa, lakini si kila ndoto ya ndoa inahusiana na jini mahaba yategemea na mazingira ya muotaji yalivyo. Ili ithibiti kama una jini mahaba yatakiwa aungaliwe kiundan ila dalili zaidi ni kuota unazaa mara kwa mara, kuota una mimba, unanyonyesha unafanya tendo la ndoa na ukajisikia raha zaid kuliko hata huyo unayeishi nae hizi ni baadh ya daliki zake na dawa yake ni kutolewa. Upande mwingine ndoto hizi zinawakilisha uaminifu kwa Mungu, vilevile ni ishara ya Jela, Madeni, kupata Huzuni, misiba, kuchanganyikiwa, kupata majukumu, nia ya kufanya mambo makubwa au kupata nafasi kubwa hapa yategemea na mazingira ya ndoto lakini pia mazingira ya muotaji. Ikiwa upo kwenye ndoa na umeota umeolewa tena kuna ishara ya migogoro na ndoa huwenda ikavunjika ikiwa hamjatafuta suluhu mapema hii ukiota unaolewa na mumeo tena haliyakuwa mpo ndoan au unaoa mkeo tena. Ukiota umefunga ndoa na mtu usiyemfahamu na hukumu

VIFUNGO NUSKI ZA KUJITIA MWENYEWE BILA KUJUA ALAF UKATAFUTA MCHAWI EPUKA MAMBO HAYA

Image
SIKU kadhaa zilizipita niliwahi kuongelea kuhusiana na madhara yampasayo mtu ambaye haogi janaba hedhi na nifasi. Niliorodhesha madhara yake na pia nikaweka muongozo jinsi ya kuoga na kujitwayarisha. Darasa zangu huwa hazimuachi mtu njia panda ukisoma unapata ufahamu na ufumbuzi moja kwa moja darasa hiI zinaletwa kwako na Mtabibu ASILI TZ. Mbali na makala hiyo pia niliweka makala ya kwanini unakoshwa unashughulikiwa lakini mambo kwakao hayakai sawa unakoshwa hata mara kumi lakini hakuana afuen jaribu kuitafuta hiyo makala usome utaongeza kitu kwenye ubongo wako lakini pia utapata point ya kuanzia kwenye kutafuta suluhu ya jambo lako. Kwa ufup madawa ya kuoga ni mengi sana siku hz kila mtu anatoa dawa sijui oga iki changanya na hiki kwanza uganga ni karama na kipaji kutoka kwa allah kitu kinachofanya kazi ni kile atakachokupa mwenyewe huyu mtaalam. Pili nuski ina vyanzo vyake sasa chakutibua ni chanzo na si kukosha mwili kwanza tibia chanzo ndo ushughulike na mwili. Leo nita

FAHAMU KUHUSU AMBARI FAIDA NA MATUMIZI YAKE

Image
AMBARI ni kitu kinachotoka katika matumbo ya samaki adimu aina ya NYANGUMI. Chenye maajabu mengi na kina gharama kubwa sana. Lakini pamoja na gharama zake pia kinafaida kubwa kuliko gharama Ambari imegawanyika katika makundi mawili kuna ambari nyeupe na ambari nyeusi zotezina kazi zake. katika kuzijua faida za AMBARI. 1):ukiiweka katika nyumba yako nyumba hiyo itakua na furaha muda wote na kheri nyingi zitapatikana nyumbani hapo na inafukuza majini wachafu na wanga na wachawi hawatakua na uwezo wa kuwachezea wala kuingia katika nyumba iyo. 2):ukiiweka katika biashara inavuta wateja na baraka zinazidi ktk biashara na inazuia majini wezi wa pesa na chumaulete. 3):ukiitaji umaarufu kuwika kutamba kujulikana kutingisha ..jifukize ambari usiku kwa siku 21 mfurulizo . 4):utajili ambari inavuta utajili kwa haraka mno .loweka ambari kwenye maji lita saba na sarafu nyeupe49 oga alfajili lita moja moja kwa siku saba na utoe sarafu saba kila siku ukatoe sadaka kwa masikini au watoto y

FAHAMU KUHUSU AMBARI INAVYOLETA MVUTO WA BIASHARA NA UTAJIRI

Image
NILIWAHI kuongelea kuhusiana na ambar na makala yangu ikakopiwa na waganga wengi wa mjini ila kubwa ninalowahusia kuweni makini katika utafutaji wa matatuzi ya shida zenu hasa wale wanaotafuta mali. niliweka makala inayohusiana na ambari. Na nikafafanua ambari ni nini na inatoka wapina nikaeleza faida zake  Pili wengi waliuziwa ambari isiyo yenyewe orijino hvyo ikawa ngumu kupata matokeo yale niliyoyaandika. Nawashaur tena somen mpaka mwisho. Leo nitaongelea kwa uchache kuhusu ambari nyeupe. Sasa hii ndo baba wa ambari na bei yake ndiyo juu kuliko ambar zote maana ambari nyeusi imeagawanyika katika mafungu mengi. Kwa kuvuta bahati ya biashara na mwili Chuukua ambari nyeupe ya mascut changanya na unga wa hardal, mringaringa  ,mpapatiko na mwita hv vnapstkana maduka dawa asili Zitwange ziwe unga kisha zigawe mafungu mawili fungu la kwanza pia utaligawa mara mbili moja utawekakwenye mafuta ya nazi yaliyoacahanganywa na karafuu fungu jingine utakuwa unaweka kwenye maji ya kuoga

FAHAMU KUHUSU TEMBO TIBA KWA WATOTO NA WAMAMA NA KUKUZA DHAKAR

Image
Tembo ni mnyama mkubwa mbugani, kwa ukubwa wake hata kwenye tiba pia anakuwa na mambo makubwa. Ukitaka uwe mkubwa katika eneo lako aidha biashara kazini eneo la michezo nk kuna vitu vya tembo hutumika kutengeneza hyo dawa njoo ofisini utapatiwa Kwa ujumla tembo ana faida nyingi. Nilishawahi kuongelea mafuta yake katika ukuzaji wa dhakari kama imekupita makala haya soma makala ya nne hapo chini kwenye ukurasa wangu nimefafanua kwa upana. Mafuta yake pia huweza kutatua tatizo la watoto waliopinda viungo wakati wa kuzaliwa ama waliovunjika huchanganywa na aina saba nyengine ya mafuta huchuliwa mtoto hii ni kwa watoto  Sasa leo ntafafanua kuhusu mavi yake tembo akishakunywa yale mavi yakikauka ni dawa nzuri kama ninavyofafanua mavi yake kwa degedege Chukua  mvuje, mavi  ya Tembo, Majani ya vitunguu saumu yaliyomenywa na watu wengi ukipata ya shughulini ni vizuri zaidi. Mfushe kwa siku tatu mfululizo mara mbili kwa siku mtoto atakaa sawa Mtoto anayelia usiku au anastuka akiwa us

SIRI NA MATUMIZI YA CHUMVI YA MAWE YA BAHARINI SEHEMU YA TATU

Image
HERI ya siku mpya mpenzi mfuatiliaji wa dondoo za afya na jinsi ya kujitibu kupitia dawa za asili na kisunna. Hii ni makala ya pili ya muendelezo wa faida zipatikanazo kwa kutumia chumvi ya mawe. Km ulipitwa pitia ukurasa wangu. Niliongelea faida mbili mapenzi na kukidhi haja leo nitaendelea na faida nyingine. Kwa ujumla chumvi ina faida nyingi sana hasa kwenye ulimwengu wa tiba kama nlvyogusa kwenye makala iliyopita halipigwi kafara bila chumvi ya mawe haisomwi albadiri bila hii kitu. MATUMIZI KATIKA ENEO LA BIASHARA Watakiwa upate maji ya kisima cha wazi lita tano chumvi kilo moja utaroweka kwa masaa saba kisha utayatumia hayo maji kupigia deki eneo la biashara hii inaendana na yale ya bahar kama nilivyoeleza kweny ile makala ya mvuto wa biashara. Pili utatfuta muita mfunguo muharaka mripu mvuma nyuki na unga wa majani ya mkomamanga utachoma eneo la biashara kwa manuizi. Hivyo vtu vnapatikana maduka ya dawa za asili popote ulipo mkoma manga unaptikana majumbani.  MATUMIZ

NDOTO ZA VITA KUPAMBANA KUSHINDWA TAFSIRI NA MAANA ZAKE

Image
TUNAENDELEA na darassa za tafsr za ndoto katika ukurasa huu wa Mtabibu ASILI TZ. Leo tunaangalia tafsri ya ndoto za vita. Hapa namjumuisaha ukiota upo vitani au uksshinda ukashindwa kuona watu wwnapambana na tafsiri zake. Vita imegawanyika katika makundi mawili kuna bdoto za majini na ndoto zinazoashiria uadui. Pia yategemea na mazingira ya muotaji na mazingira ya ndoto. Mfano kama ni Askari au Mwanajesh ni kawaida kuota upo vitan au kupambana na watu kutokana na asili ya kazi yako. Ikiwa unaota upo vitani mara kwa mara unapambana kisha maisha ya kawaida ukawa unapenda sana ugomvi mtu wa hasira sana ni dalili za jini MAKATA. Moja ya dalili nyengine za jini huyu ni kuhisi kuungua kwenye nyayo, uke/uume, tumbo, kichwa na sehemu zingine za mwili. Wasiwasi wa moyo na kujiona kama unafariki wakati wowote. kuishiwa na damu mara kwa mara bila sababu za kimsingi na za kisayansi. Wakati mwingine kutokwa na vipele venye kutoa harufu mbaya vinapopasuka na unaeza ukawa na dalili zote z

KISENYA KUNI, KUMBA NYASI ANAVYOTUMIKA KWENYE SHIDA MBALIMBALI KWW TIBA ASILI

Image
HUWENDA usifahamu jina lake kati ya haya niliyotaja. Pia huwenda kilugha chenu au eneo mnaloish mnafahamu kwa jina jengine tifaut lakin picha itoshe kukuonesha na kufahamu kuwa tunaongelea mdudu wa aina hii. Anaitwa kisenya Kuni au Kumba Nyasi na majina mengine mengi. Mdudu huyu anatabia ya kujijengea kijumba chake kisha huishi ndani ya hicho kijumba. Wapo wanaotengeneza kwa kutumia nyasi, pia wapo wanaotumia vimiti kutengenezea nyumba zao. Moja ya tabia zao wanauwezo wakukaa ndani ya jumba kwa muda mref na hutoka pale anapohitaji kitu maalum.  Huwa wanatembea na nyumba zao ikifika kipindi huziacha na kutengeneza nyumba mpya, kama unaish shamba ulishawah kukutana nyumba tupu ya mdudu huyu basi ujue ameamua kutengeneza mpya au ameuawa alipotoka. kama utamkanyaga mdudu huyu kwambahat mbaya bimaana bila ya kumuona unapotea uendapo na unaweza ukaipita nyumba yako hata mara tano pasina kuijiua. hadi atokee mtu akustue au ubadilishe nguo nje ndani. Mdudu huyu ana faida nyingi san

BALAA NA MATUMIZI YA AMBARI NYEUSI KATIKA ULIMWENGU WA KIZA

Image
NILIWAHI kuzungumza ambari kwa ujumla, pia nikaweka darassa linalohusu ambari nyeupe. Nilifafanua faida zake na matumizi yake katika tiba mvuto wa biashara na kulinda mali ikiwa ulipitwa pekua post zilizopita. Nilipokea oda nyingi za ambar waliopata walishukuru lakini pia nilipokea malalamiko kuwa ambar walizonunua madukan nyingi hazikuleta majibu yale niliyoyasema. Kwenye ile makala nilieleza kuwa ambar yenyewe halisi huwez ipata kwa bei rahisi, sasa mtu kauziwa ambar elf tano, elf 30 au elf 50 hiyo automatic ni fake. Pia wapo wanauza ambar bei ghali lakini pia sio halisi cha muhimu ni kuwa na makini fika kwa watu wanaoaminika katika maeneo unayoishi ambao unajua watakusaiaidia kiwepesi. Sina maana kwamba madukan hakuna ambar halisi lahasha. Leo tuangalie ambari nyeusi, hii imegawanyika katika mafungu mengi lakini hapa nitaeleza kwa ujumla baadhi ya matumizi ya ambari nyeusi. Hii hutumika sana katika shughuli za kupiga vitu na kuondoa vtu vigumu. Hii ikiwekwa kwenye kuroge

KWANINI HUFANIKIWI MAJAMBO YAKO NA USHASHUGHULIKA SANA, FAHAMU UNAPOKWAMA

Image
WATAALAM wengi hukupa dawa kutokana na maelezo yako hasa wataalama wa mjini hawasumbui vichwa kujua tatizo. Pia wengi wao ni watu wakunakilinakala za wngine na kuweka kwenye page zao yaani copy and paste. Nuksi inajulikana kwa maelezo tu mtu akijieleza wajua hii ni nuksi sasa kinachotakiwa ni kujua chanzo cha nuksi na utibie chanzo. Katika mambo yanayoweza kukwamishwa vitu visitimie vipo vingi na kila jambo lina matatuzi yake kitiba na mafanyo. Mfano kuna nuski, vifungo, nadhiri, husda, radhi, uchawi, jini mahaba, majini maiti pamoja na mambo mengine, hapa nmetaja kwa uchache lakini kuna mambo mengi sana yanayoweza kukukwamisha. Mfano ulikuwa huzai ukasema neno mimi ikotokea nimezaa nitachinja mbuzi na ukalirejea hilo neno mara kadhaa aidha ulipokuwa unatumia dawa au katika maombi ikitokea umezaa hujachinja mbuzi mawili wewe au mtoto mambo yake yatakwama hasa ni wewe mtia nia.  Sasa hili dawa yake si kukoshwa wala makafara tafuta mbuzi achinjwe utasema tu yale maneno uliyot

NDOTO ZINAZOASHIRIA KUWA UNA MAJINI WAZURI, WABAYA WAKICHAWI NA HATUA ZA KUCHUKUA

Image
UHALI gani mpenzi mfuatiliaji wa darasa zangu zinazohusiana na nyota, ndoto uchambuzi wa miti na mambo mengine ya kidunia. Leo nakultea tafsir ya ndoto zinazoashiria una majini yawe wema au wabaya  utajuaje katika ndoto na baadhi ya dalili zake anayekuletea darasa hizi ni Mtabibu ASILI TZ. Kwanza kuna ukoo una isimu ya majini ya uganga. Namaanisha kuna familia wana historia ya kuwa waganga kuna watu walipita kabla yako aidha uliwaona au uligadithiwa walikuwa waganga. Pia kuna isimu za koo nyenginr ni Uchawi na wengine wana isimu za usharifu sasa kila mmoja ana dalili zake katika ndoto. Lakini pia kuna majini ambayo yanatumwa kuja kusulubu watu aidha ulihombana na mtu au unaringa sana. Ukiota umeingiwa na kitu mwilini aidha nyoka simba au mnyama yoyote au upepo unekuvaa mwilini. Au unaweza ukaona kabisa umekaa pahala au unatembea ghafla kitu kikakuvaa kisha maumivu yakaanza mwilini. Mwili kukosa nguvu vitu kutembea kujihisi kichefuchefu unaweza pima hospital usiw

VITU VYA KUZINGATIA KATIKA BIASHARA ILI KULETA MVUTO WA WATEJA NA KUJIKINGA NA WEZ

Image
JUMA lililopota nilizungumzia kuhusiana na nyota za uzawa na uchambuzi wake. Nilichambua kuhusiana siku, rangi, pete za bahati. Pia nikakugusia biahsra au kazi na vipaji vya kila nyota husika halikadahalika nikazungumzia rangi kwa ajili ya biahsra na mafusho yake na muda wakuyachoma kama umepitwa zitafute kwenye post zilizopita. Makala hii ni ya pili ambayo naitoa kuhusiana na masuala ya mvuto wa biashara. Leo nitagawa mafungu mawili ya biashara zile za kutembeza  na zile za kwenye frem, jitahidi kusoma kwa umakini zaidi na kufuata kile nitakachokiandika. Zakutembeza nazijumlisha na na wale wanaofanya biashara kwenye mitandao ni sawa tu na wale wanaotembeza. Hawa sasa jinsi kufanya ili biashara yako iwe na mvuto fuata maelezo yafuatayo. Kwanza wewe mwenyewe uwe na mvuto bimaana usiwe na nuksi mikosi wala hasadi hapa inakupasa utumie dawa za mvuto kulingana na nyota yako ili kukupa mvuto zaid hapa ndio utafahamu kulpitia zile darasa za nyota nilizungumzia mafusho. Pili unata

JINSI YA KUTEGUA MITEGO YA MALIMBWATA

Image
KUNA malalamiko mengi ya watu wengi humu wakilalamika juu ya darassa na mapokeo umya wanawake wanavyofundishana juu ya kudhuru waume zao ambao ni sisi wanaume. Leo nitakupa njia za kujiepusha nazo hivyo hvyo vtu lakini pia nitakuwa nawapa baadhi ya mitego yao wanayowafanyia. Mtego wa kwanza wanahamasishana kufuga mavuzi yao. Ukiona mtu wako anayafuga haya kwa wingi ujue kuna kazi yake maalumu. Siku yake ikifika hunyolewa na hukaangwa kwenye chungu ili apate unga wake huchanjwa sehem za mbele kwao kwa manuiz. Pili unawwza ukawekewa kwenye chakula au kinywaji kwa manuiz huchomoki. Sasa hizi mambo huzaa sihiri mwilini yaani huzaa uchawi ambao wengi baadae mnalalamika hamna nguvu za kiume. Mkitoka nje kwenye nyumba ndogo wengine hawasimamishi kabisa au husimama legelege, ni moja ya dalili za kuathirika na hvyo au wakat mwingine huchukia wanawake hata mtoto awe mkali vp anakushobokea lakini huonyesh ushawishi ujue ushapigwa pini. Kuna mti unaitwa mvuma nyuki angalia pichani mizi

NDOTO ZA KUWAONA, KUPIGANA KULA NYAMA YA PAKA MAANA NA HATUA ZA KUCHUKUA

Image
LEO tunazungumziw ndoto zinazohusiana na mnyama Paka. Tumezoea kuwaona Paka majumbani mwetu kwan ni mnayama afugwae hasa kwa watu wa imani ya dini fulani ambao wanaishi ukanda wa Pwani kufuga mnyama huyu kwao ni moja ya ufahar wao. Pia utandawazi umekuja kufumbua macho watu kwan siku hizi kumekuwa na wafugaji wengi wa paka wengine hata wasijue maana ya kufuga mnyama huyo humtumia kama Pambo la nyumba tu. Paka hutumika kukimbiza Panya nyumba yenye paka panya hawakai, kuna nadharia kuwa paka hutumiwa na wachawi ina ukweli japo sio wote wachawi wanauwezo kujibadilisha kwenye umbile la paka pale wanapotaka kufanya mambo yao mchana, na si paka tu umbile lolote wanalotaka hujigeuza kwa msaada wa jini wao wanayemtumia. Leo tuangalie tafsiri za paka, ukimuona paka ndotoni ni ishara ya Mwizi, Ugonjw, Unyonge na wakati mwingine pia huwa Faraja inategemea n mazingira ya muotaji na aina ya ndoto uliyoita siku hiyo.  Ikiwa umeotaPaka ameingia ndani ya nyumba jua humo yumo mwizi. Kwenye

MADHARA YA UCHAWI WA MAPENZI UNAVYOLETA SIHIRI NA KUKUFUNGA

Image
NILIWAHI kuzungumza kuhusiana na madhara ya malimbwata nikfafanua jinsi mfanyiwa anavyoweza kuathirikia na malimbwata kiakili na kiafya. Leo tuzungumze kiundani uchawi wa mapenzi. Zile darassa za mitego ya uchawi kwa hapa nimeshazinaliza zitaendelea kwenye group sasa tunaingia kwenye madhara ya uchawi wa mapenz anayekuletea darasa hizi ni Mtabibu ASILI TZ. Uchawi huu huathiri nyota afya hata ufanyaji jimai 'tendo la ndoa' kiwango kinashuka. Yategemea na ulivyofanyiwa na maagano kati ya mfanyaji mtaalamu wake. Hapa kinachokudhuru ni dawa na matamshi yale atakayotamka mfanyaji wa dawa husika.    UNAWEZAJE KUROGWA KIMAPENZI. Kwenye maisha ya kawaida yaweza akatokea mtu akawa anakuhitaji kimapenzi ila ukamkataa. Ikiwa mtu huyu si mchawi hakuna tatzo kubwa wala uchawi mkubwa utakaokukuta yeye ataenda kwa mtaalam atasema namtaka fulan awe wangu kwa lengo zur tu lakini yeye hanitaki. Au mlikuwa na mahusiano ghafla mawasiliano hufanyika kazi za kuvuta karibu huyo mtu na kum

UCHAMBUZI WA NYOTA YA SAMAKI, RANGI, SIKU, PETE ZA BAHATI, MAFANIKO NA MAPENZI

Image
HII ni makala ya mwisho katika mfululizo wa makala 12 ambazo niliziahidi kutolea ufafanuzi wa nyota. Ufafanuzi ambao ulihusiana na rangi za bahati siku pete za bahati mafanikio katika biashara mali na mapeniz. Na hii ndio makala ya mwisho ya uchambuzi na leo nazungumzia nyota ya Samaki, makala hizi zinaandaliwa na Mtabibu ASILI TZ. Ikiwa umepitwa na hizo makala kumi na moja soma post zilizopita kupitia ukurasa wangu ili ujue nyota yako na uchambuzi wake kwa kina. Ukihitaji uchambuzi binafsi utachangia gharama za uchambuzi hii namaanisha wale wanaotaka kuchambuliwa inbox hivi vtu kwa kina itakupasa utoe ujira. Samaki ni nyota ya 12 katika mlolongo wa nyota 12. Nyota hii ni kwa watu waliozaliwa kati ya Tarehe 19 Februari na Machi 20. Ufafanuzi ni watu waliozaliwa kuanzia tarahe 19, 20,21,22,23 mpaka mwisho wa mwezi Februar na kuanzia tarahe 1,2,3,4 mpaka tarahe 20 mwezi March. Wale wasiojua tarehe zao ni watu au wenye majina yalio anza na herufi L na X na  wote ni Nyota ya Sa

UCHAMBUZI WA NYOTA YA NDOO, SIKU, SAA RANGI, PETE ZA BAHAT, MAFANIKIO NA MAPENZI

Image
AHLAN WASAHALA mpenzi mfuatiliaji wa darasa za ndoto nyota miti na mambo mengine yakidunia kwa madawa ya asili. Leo tunaendelea n uchambuzi wa nyota ya Ndoo anayekuletea darasa hizi ni Mtabibu ASILI TZ. Hii ni nyota ya kumi na moja katika mlolongo wa nyota 12. Nyota hii ni kwa watu waliozaliwa kati ya Tarehe 20 Januari na Februari 18. Ufafanuzi ni wale waliozaliwq kuanziw tarahe 20,21,22,23,24 mpaka miwsho wa mwez Januar na kuanzia tarahe 1,2,3,4 mpakq tarahe 20 mwez February. Pia wale wenye majina  yalio anza na herufi K, W, H lakini hawa hawajui tarahe zao za kuzaliwa ikiwa unaijua tarehe yako fuata tarahe yako.     ASILI, RANGI, SIKU NA PETE BAHAT Asili yao ni Upepo.Malaika wake anaitwa  Kafyaeel, na Jini wao anaitwa Abuu Nuhu, Sayari yao ni Uranus. Siku yao ya bahati ni Jumamosi. Namba yao ya bahati ni 8 Rangi zao ni Bluu, Kijivu na Samawi ya Bluu. Wenye nyota ya Ndoo wanatakiwa wapake nyumba zao au magari yao au sehemu zao za biashara rangi zilizotulia kama Bluu au Kij

MITEGO YA KICHAWI, FEDHA YAKO INAVYOWEZA KUTEGWA NA KUFILISIKA AU KIFUNGWA BILA KUJIJUA

Image
LEO tunaingia mtego wa pili wanaotumia wachawi katika kudhuru watu na hiiinahusiana na fedha yako yako mwenyewe na utawapa mwenyewe kwa mkono wako. Jana tulizungumzia mitego ya nyoka jinsi unavyoweza kuiingia na namna ya kuepukana nayo kama ilikupita angalia makala ya jana. Katika kipengele cha kuingia kwenye uchawi leo tutazungumza kuhusiana na kuingizwa na marafiki au jamaa zako wa karibu. Hii ina tofaut kidogo na kurithi kwa sababu kurithi unachaguliwa moja kwa moja kuwa mrithi wa kiti yaan ukiingia na cheo unapewa kila cha mtu wako aliyekurithisha.   Kuingizwa inakuwa kama vile unavyojiingiza kwenye makundi na rafiki zako. Mfano ukiwa na marafiki wanaopenda kukopa mikopo nasi kuna uwezekano mkubwa wa wewe kuingia kwenye mkumbo huo. Hii huanzia kwenye ndoto utakuwa na mfululizo wa ndoto za kuwa upo kwenye sherehe, mnakula vyakula vya kila aina, unakuwa kama mgeni mualikwa kila mtu anataka ukaribu na wewe kwenye hizo ndoto. Ikiwa hizi zinakujia mara kwa mara ni ishara moj