HUSDA NI NINI NA HASIDI NI NANI NA UTAJUAJE KAMA UMEHUSUDIWA FAHAMU KIUNDAN NANJINSI YA KUJIEPUSHA NA HUSDA.



KARIBU tena kwenye mfululizo wa darasa zangu kupitia ukurasa huu wa mtabibu asili tz, kuna baadhi ya watu wamekuwa wakikopo darasa hizi na kuweka kwenye kurasa zao sio mbaya maana unaonyesha heshima kwangu kuwa nafanya vtu vinavyowavutia wataalam na watu wasio na utaalam ila unachotakiww chini ya makala yako uandike kuwa umeitoa hapa hii ni heshima lakini pia itakufanya uwe huru kuendelea kuzitumia makala zangu.

huu ndio mmea wa mkunazi wenyewe unaozungumziwa 

Leo nitauna kisa kimoja kimezungumza kuhusiana na husda hasidi na mtu aliyefanyiwa husda anakuaje. Husda ni Hasidi ni mtu amabye anamuomea choyo mtu aliyejaaliwa kitu fulan ambacho aidha yeye anacho au hana na anataman yule mwenziwe asiwe nacho. Kifupi hasidi ni mtu anayetaman neema mwenzie iweze kuondoka.

Hasidi wapo wa aina mbili aina ya kwanza hawa ni wagonjwa yaani unaumwa husda kwa lungha nyepesi inaitwa kijicho. Yaani mtu anaweza akakitazama kitu kiharibia au mtu akimuangalia basi ataumwa lakini asikusidie ubaya. Pia katika kinywa chake akitamka kitu lazima kitokee mfano utasikia mtaan bibi fulan mdomo wake hauend bure akikuambia utaona bas utakutwa na mabalaa.

picha ya majani ya mkunazi kwa ukaribu

Sasa huyu anaumwa husda yaan ana mashetan mabaya kwenye mwili wake ambao wanakuwa wanamtumia kwenye mambo ya husda. Mfano anaweza akamuangalia mgonjwa akazidi kuumwa au akafa. Kuna kijiji fulan iliwah kutokea kuna mtu alikuwa haruhusiki kwenda kuangalia wagonkwa kwa sabab ya kijicho lakini yeye si mchawi. Huyi sasa anatibika kama akitaka mwenyewe anaondolewa wale majini wa husda.

Hasidi wa pili ni wale wakudhamiria kabisa kwamba wewe umeoa au kuolewa yeye anaumia moyoni kwann fulan apate ndoa kwan fulan ajenge nyumba kwann fulan afanye biashara kwann fulan azae. Sasa huyu hasidi ana sehemu tatu za kukuumiza kwanza anaanzia macho akishaiona rehma uliyojaaliwa anahamishia kwenye mdomo ataanza kukusema kwa wwtu kuwa unaringa.

picha ya majani ya mkunazi kwa karibu

Akiihimishia kwenye mikono ujue ni utendaji sasa anaenda kukushughulikia ili hata hicho kidogo ulichonacho kikutoke ili ubaki mtupu apatr kufurahisha nafsi yake. Hata mtu akikusaidia alaf akawa atangaza ule msaada wake kiubaya yaan bila mm yule fulan asingefanikiwa msimuone vile huyu pia hasidi.

Na husda mbaya ni ile inayofanywa na watu wako wa karibu aidha mkeo, mume, ndugu wa damu ambao wanakujua vzur hawa ndio wanaweza kukuumiza zaid kuliko mtu wa kando sababu hawa wanaweza wakakupa husda na vifungo jui yake.

Unaweza mtu ukawa na mali ikaondoka ghafla ukamiliki gar likawa linaharibika unaweza ukanunua kuku kabla hujampika akaharibika. Unaweza ukatolewa posa muoaji akaingia mitini asirejee tena.

Dalili za aliyehusudiwa kupata kichefuchefu cha mara kwa mara ukpima huna maradhi, kukonda bila sababu za msingi, kuhisi hasira kuwa mpweke wakat mwingine hujiliza pasina sababu. Kutokuwa na hamu au kuchukia kufanya kazi. Wakat mwingine huwachukia mpaka watu wanaokushaur kuhusu kazi. Watu kukudharau kutokuwa na iman na wewe hata ishu za kushika fedha huwez aminiwa moja kwa moja.Husda ikikomaa husababisha maradhi ya ukoma

Kila chanzo cha husda kina tiba zake na tatizo likaisha na mambo yako yakaenda sawa. Kujikinga au kuvunja husda za vijicho hizi sio zile za kitendewa ni zile za kijicho tafuta majani ya mkunazi mabichi 2. Fikicha hayo majani kisha weka kwwnye chupa ya maji lita moja na nusu au mbili kaa chini utulie jitenge na watu utafute pahala palipo tulia kisha fuata utaratibu ufuatao.

Fungua ile chupa kisha mdomo wako uelekee kwenye mdomo wa hiyo chupa soma ayyatul kurusiyu 1,  ukinaliza kusoma puliza yale maji mara tatu. Somea surrat Jinni kul uhiya mara moja kisha puliza tena mara tatu soma surrat lkafiruni mara moja kisha utapuliza mara tatu, surrat Ikhlas mara moja kisha utapuliza mara tatu, Surrat Falaq mara moja kisha utapululiza mara tatu na Surrat Nnas kisha utapuliza mara tatu. Wakati unasoma hutakiwi kuzungumza na mtu hata kama ukiwa umechoka jipumzisha mwenyewe usizungumze na mtu

Ukimaliza utayagawa hayo maji mara mbili nusu utakuwa ukichanganya na maji ya kuoga na nusu utakuwa ukichanganya na maji ya kunywa fanya kwa siku saba.
Njia ya pili kama utakosa mkunaz unaweza chukua bakuli la maji la lita tatu tia udhu uwe msafi jitenge na watu wakati unataka kufanya kazi yako usiruhusu hata kuongea na simu kaa chini na bakuli lako kisha fuata maelezo.

Somea hayo maji surrat fatiha mara 41, soma maneno haya la ilaha ila anta subhanaka inni kuntu mina dhwalimiyn mara 41, kisha surrat falaq mara 7 kisha utasoma surrat nnas mara saba utayatumia kuoga kwa siku 7 mara mbili kwa siku.

Husda ya ndugu haikuanza leo toka enzi za Nabii Adam radhi za mwenywzi mungu zimuendee juu yake, pia wakati nabii Yusuf alihusidiwa nduguze baada ya kupata ndoto ambayo ilimtafairi baadae atakuja kuwa mtume wa mungu. 
 
Vipo vifa vingi kwenye Quran vinavyoeleza husda na mdhara yake. Kwa ufupi hasidi ni adui wa Mwenyezi Mungu kwasababu huingilia mipaka ya ridhki anayoitoa yeye kwa mja mtakae.

Kuna husda za majini husda za wanaadamu na husda za kichawi sasa hizi zikionhozana zikakutana ndio ukipita watu wanakuona kama mtoto mdogo au mwendawazimu waweza dharauriwa hata mkeo nyumban

Kupata dawa kutoa hasadi

Una tatzo lolote la afya nyota nguvu za kiume, uzazi biashara kesi kuibiwa kuuza nk kwa dawa na mafanyo niachie ujumbe inbox
+255621442936

Whtsp group ni la malpo kwa wanaohtaji

Comments

Popular posts from this blog

MAFUSHO MADINI YA KILA NYOTA NA JINSI YANAVYOTUMIKA

NDOTO ZA FEDHA NA TAFSIRI ZAKE UKIOTA UMEOKOTA HELA. UKIOTA UMEDONDOSHA HELA. UKIOTA UNAPEWA HELA

FAHAMU KUHUSU MTI NDULELE TURA FAIDA NA MATUMIZI KATIKA AFYA NA MAPENZI